Senegal imepiga marufuku usambazaji wa jarida hilo kote nchini humo
Raia wengi wa Senegal ni waisilamu ambao bila shaka watafurahishwa na hatua hii ya serikali.
Nchi
hio pia ina uhusiano wa karibu na Ufaransa ambayo ilikuwa mkoloni wake
na majarida mengi ya kifaransa yanapatikana nchini humo.
Jarida
hilo limesambazwa kote duniani likuwa na kibonzo kinachomkejeli mtume
akionekana kulia huku akishika bango linalosema ''Mimi ni Charlie'' huku
kichwa kinachofuata kikisoma, '' Yote yamesamehewa''.
ni hatia
kwa yeyote kusambaza au kuchapisha kibonzo kilicho kwenye jarida la
Charlie Hebdo kote nchini,''ilisema taarifa ya shirika la habari la APS
likinukuu taarifa kutoka kwa wizara ya mambo ya ndani.
Mwandishi wa BBC nchini humo, Mamadou Moussa Ba anasema hakuna cha kushangaza kuhusiana na marufuku hio.
Raia
wengi wa Senegal wamemkosoa rais Macky Sall kwa kuhudhuria maandamano
nchini Ufaransa kuonyesha umoja kufuatia mauaji ya wachora vibonzo wa
Charlie Hebdo na vijana waisimalu waliosema kwamba walikuwa wanalipiza
kisasi kibonzo kilichochorwa awali na jarida hilo pia kumkejeli mtume.
Gazeti moja nchini Kenya, la The
Star limeomba radhi kwa kuchapisha ukurasa wa kwanza wa jarida la
Charlie Hebdo uliokuwa na kibonzo kinachomkejeli mtume Muhammad.Wahariri
wa gazeti hilowamesema kuwa wanaomba radhi ikiwa walimkera mtu yeyote
kwa kuchapisha ukurasa huo. Malalamiko kutoka kwa viongozi wa kiisilamu
yalipelekea wahariri wa gazeti hilo kuomba radhi.
No comments:
Post a Comment