Wezesha

kama una maoni au habari tafadhali tutumie kwa kupitia email yetu.shanellally@gmail.com

Thursday, 29 January 2015

KESI YA PONDA TENA FEBRUARY


Akitoa ushahidi wake mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, Mary Moyo shahidi Jafert Kibona, ambaye wakati huo alikuwa Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Morogoro, alisema Agosti 9, 2013, polisi walipata taarifa kuwa, Sheikh Ponda angekwenda Morogoro kwenye kongamano, hivyo waliwataka waandaaji kumsalimisha polisi kiongozi huyo.
Kibona ambaye kwa sasa ni Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Mtwara, alisema polisi walimtaka Sheikh Ponda kujisalimisha kutokana na kutafutwa kwa tuhuma za kutoa maneno ya kashfa na uchochezi, Dar es Salaam na Zanzibar.
Hata hivyo, Sheikh Ponda alikaidi amri hiyo, badala yake aliendelea kutoa maneno ya kashfa na uchochezi katika kongamano la Morogoro, alidai shahidi huyo mahakamani hapo.
Alidai walishindwa kumkamata Ponda baada ya wafuasi wake kumwingiza kwenye gari dogo na kumtorosha, kabla ya kupata taarifa kupitia mitandao ya kijamii kuwa kiongozi huyo alijeruhiwa kwa risasi bega la mkono wa kulia.
Kibona alisema walikwenda Hospitali Mkoa wa Morogoro, lakini hawakumkuta Ponda na siku iliyofuata walipata taarifa kuwa amelazwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Wakili wa utetezi, Juma Nassoro alimuuliza shahidi huyo kuhusu mtu aliyempiga risasi Ponda, ikiwa polisi ndiyo pekee waliokuwa na silaha siku hiyo.
Aliuliza pia kwa nini polisi walishindwa kumkamata Ponda wakati hakuwa na silaha. Kesi itatajwa tena Februari 2 na 19 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment