Wezesha
kama una maoni au habari tafadhali tutumie kwa kupitia email yetu.shanellally@gmail.com
Sunday, 28 June 2015
LOWASSA AZOA WADHAMINI WENGI DAR
Sunday, June 28, 2015
Mafuriko Ya Lowassa Yatua Jijini Dar......Kingunge Amwaga Wino Hadharani Kumdhamini, WanaCCM 212,150 Wajitokeza Kumdhamini
WAZIRI Mkuu wa zamani, Edward Ngoyai Lowassa amepata udhamini wa kishindo katika mkutano uliofanyika jana katika ofisi kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kinondoni.
Lowassa alipata udhamini huo baada ya wanachama kujitokeza katika ofisi za Makao Makuu ya CCM ya Wilaya ya Kinondoni, Mkwajuni, Dar, ambapo alipata zaidi ya wadhamini 212,150 huku akisema Dar imevunja rekodi ya mikoa yote ya Tanzania.
Akizungumza na maelfu ya wananchi waliofika katika mkutano huo Lowassa alisema kuwa amefurahishwa na watu waliojitokeza kumdhamini kwa kishindo kikubwa na hivyo hatavunjwa moyo na maneno ya watu yanayovumishwa kuwa anawapatia fedha ili wafike kwenye mkutano wake .
Lowassa aliongeza kuwa anawaomba Watanzania wampe ridhaa ya kuwa rais wao kwani atahakikisha mianya yote ya rushwa na utendaji mbovu wa kusuasua anausimamia kwa haki na weredi na ndani ya miezi sita tayari matokeo yatakuwa yameonekana.
“Nawaombeni wananchi mnipeni ridhaa ya kuingia ikulu yaani nitahakikisha mianya yote ya rushwa na ufisadi nautokomeza, muyapuuze maneno na minong’ono ya watu kutaka kunichafua,” alisema.
Chini picha za matukio
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment